FIFA YAMKALIA KOONI RAIS WA SOKA HISPANIA

Zurich

Shirikisho la soka Duniani, FIFA,linapanga kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya Rais wa Shirikisho la soka nchini Uhispania ,Luis Rubiales, kutokana na kitendo alichokionesha wakati wa fainali ya kombe la Dunia la Wanawake siku ya Jumapili.

Rais huyo alimbusu mchezaji wa Timu ya Taifa ya Uhispania, Jenni Hermoso ,mdomoni wakati wa hafla ya kukabidhi tuzo kwa washindi, mara tu baada ya Uhispania kuishinda Uingereza.

FIFA itafanya uchunguzi hili kubaini iwapo vitendo hivyo vinakiuka kifungu cha 13 cha kanuni za nidhamu ,ambacho kinalenga tabia yenye kuudhi na uchezaji wa haki.

Kanuni inasema, hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya yeyote anayekiuka “kanuni za msingi za tabia njema”kumkosea heshima mtu au mwanasheria kwa njia yoyote haswa kwa kutumia ishara au lugha yenye kudhalilisha au “kuonyesha tabia yenye kuharibu sifa ya mchezo wa mpira wa miguu au #FIFA”

Loading

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV

Related News 📫

THINGS YOU MUST NOT DO DURING SEX
16 THINGS YOU MUST NOT DO DURING SEX Looking at time...
Read more
MANCHESTER CITY have been FINED over £2million...
The Premier League released a statement to reveal the champions...
Read more
LOWASSA HATUNAE TENA
MAGAZETI
Karibu Mtanzania popote pale ulipo kwenye asubuhi ya leo...
Read more

Leave a Reply