Habari Kuu
Waziri wa Fedha ,Dkt .Mwigulu Nchemba ,ameiomba Benki Ya Dunia kuharakisha upatikanaji wa Dola za Marekani zaidi ya Milioni 500 ifikapo Novemba 2023 ili zisaidie kukabiliana na uhaba wa Fedha hizo katika mzunguko wa Fedha Nchini.
Dkt. Mwigulu ameuambia ujumbe wa Benki ya Dunia (WB) unaosimamia kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika kuwa changamoto ya upatikanaji wa Dola inachangia Mfumuko wa Bei na kukwamisha uagizaji wa Bidhaa muhimu ikiwemo Mafuta.
Aidha,amesema Serikali kupitia Bunge imefanya maboresho na kupitisha Mabadiliko mbalimbali ya Sheria na kanuni zitakazowrzesha kuvutia Uwekezaji wa Mitaji na Teknolojia.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.