BENZEMA ATISHIWA TENA

0:00

MICHEZO

Kufuatia shutuma za Waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa, Gerald Darmanin, kuwa Karim Benzema “ana uhusiano ” na kundi la kigaidi la Muslims Brotherhood, seneta wa Ufaransa Valerie Boyer ,ameibuka na kutoa kauli tata dhidi ya Mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid.

Kupitia taarifa kwenye vyombo vya habari, Seneta huyo ametaka hatua kali zaidi zichukuliwe dhidi ya Benzema, ikiwa tuhuma za kujihusisha na kundi la “Muslims Brotherhood ” zitathibitishwa kutoka kwa Waziri huyo wa mambo ya ndani.

Kwenye taarifa hiyo ,Seneta Boyer alisema,

“Kama kauli za Waziri wa Mambo ya Ndani ni kweli, lazima Karim Benzema awekewe vikwazo “.

“Kwanza Benzema apokonywe tuzo yake ya Ballon dOr,lakini pia,ni lazima mchezaji huyo avuliwe uraia wa Ufaransa. Hatuwezi kukubali Mfaransa mwenye uraia pacha ,na kujulikana kimataifa, atuvunjie heshima na kuisaliti nchi kiasi hiki”.

Mjjadala na tuhuma hizo imeibuka baada ya Benzema kukaa kimya kwenye shambulizi la kigaidi lililohusisha mauaji ya mwalimu Ufaransa nje ya mji kidogo wa Paris, huku siku chache baada ya tukio hilo,Mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid alitumia kurasa zake za mitandao ya kijamii kutoa pole kwa raia wa Palestine huku akitaka haki itendeke.

Loading

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV

Related Posts 📫

Sheggz shares how he handles interested ladies...
CELEBRITIES Sheggz, a reality TV star, has revealed how he...
Read more
WHY MEN NEED TO LEARN ABOUT WOMEN
Women fall in love with words. Words communicate your intentions...
Read more
Our target was to finish top of...
The Zambia Men’s National Team have concluded their 2025 Africa...
Read more
Muchova stuns Sabalenka, Zheng beats Andreeva in...
Karolina Muchova snapped U.S. Open champion Aryna Sabalenka's 15-match win...
Read more
UTI KWA WANAUME
Uti kwa wanaume maambukizi ya mfumo wa mkojo kwa wanaume...
Read more
See also  MESSI NA RONALDO KUKUTANA UWANJANI

Leave a Reply