JINSI YA KUFAHAMU UNAYEMPENDA NAE ANAKUPENDA PIA

0

0:00

MAPENZI

Imekuwa ni jambo gumu kufahamu ni kweli mtu unayempenda kama nae anakupenda pia? Leo ,kwa ishara hizi basi utaweza kufahamu vizuri nafasi ya mwenza wako kwako.

ā¤

1. Sio mtu ambaye anaweza kufanya jambo ambalo linaweza kuhatarisha uhusiano wenu.

2. Sio mtu wa kuanza kukufikirisha mara mbili mbili au kukupa maswali moyoni

3. Ni mtu anayekukubali kwaajili ya kila kitu chako lakini akifahamu fika una mapungufu lakini yeye anabeba mazuri yako pekee na kuona mapungufu yako sio mapenzi.

4. Ni mtu anayekwambia ukweli badala ya kukupamba maana anakupenda.

5. Ni mtu anayekufichia madhaifu yako hasa likitokea jambo kubwa mbele ya watu na baadaye atakuelekeza cha kufanya mkiwa wawili nyinyi pekee.

6. Ni mtu ambaye mara nyingi atakubebea zawadi, atapenda mtoke wote na kila mara ni mtu wa kukutania

7. Ni mtu anayekwambia una umuhimu gani kwenye maisha yake ya kila siku.

8. Mapenzi siku zote yapo kwenye mambo madogo madogo ,kwahiyo yeye hata kwa jambo dogo ataliona kubwa.

9. Ni mtu wa vitendo na sio maneno tu kwani anajua fika maneno hayajengi ghorofa.

10. Ishara zake zote za mapenzi zinakuonyesha au zinagusa hisia zako . Busu lake au anavyokukumbatia inakuonyesha kweli huyu mtu anakupenda pia.

11. Ni mtu ambaye anaweza kukupa nafasi au uhuru unapokuwa hauko vizuri kiakili,kiafya au kiuchumi. Kiufupi, ni mtu anayejali.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading