WATOTO WA MR IBU WAIBA PESA ZA MICHANGO YA MATIBABU
NYOTA WETU.
Polisi wanawashikilia watoto wawili wa msanii maarufu wa Nigeria mwigizaji, John Okafor maarufu Mr Ibu kwa madai ya kuiba Tsh 153 fedha za michango ya matibabu ya Mr Ibu ,na kujaribu kutorokea nchini Uingereza.
Onyeabuchi Okafor na Jasimine Okekeagwu wanadaiwa kudukua taarifa za kibenki za Mr. Ibu na kuiba fedha hizo ambazo ni kwaajili ya matibabu ya nyota huyo ambaye aliugua kwa muda mrefu na kuomba kuchangiwa matibabu yake baada ya kukatwa mguu mmoja.
Aidha,kati ya fedha hizo mamlaka imefanikiwa kurudisha takribani milioni 139 huku watuhumiwa hao wakiachiwa kwa dhamana huku wakitarajiwa kufikishwa Mahakamani Machi, 2024.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.