ALEX IWOBI ASHAMBULIWA

0:00

MICHEZO

Baadhi ya mashabiki wamekuwa wakimsakama , Alex Iwobi (27) ,kwenye mitandao ya kijamii ,wakimlaumu kwasababu ya timu yao ya taifa kupoteza mchezo wa fainali dhidi ya mwenyeji Côte d’ivoire.

Alex Iwobi, ambaye alitolewa uwanjani dakika ya 79 na mchezaji mwenzake Alhassan Yusuf kuchukua nafasi yake.

Kutokana na mashambulio kwenye mitandao hiyo ya kijamii, Mchezaji huyo alilazimika kufuta picha zake zote kwenye mitandao yake ya kijamii mnamo siku ya Jumatatu Februari 12,2024.

Nahodha wa timu ya Taifa ya Nigeria 🇳🇬, Ahmed Musa na baadhi ya Wanigeria wamemtetea Iwobi na kusema sio haki kumlaumu mchezaji huyo pekee.

“Wapendwa mashabiki, naomba nitoe wito wa kuacha unyanyasaji wa kimtandao dhidi ya Alex Iwobi.

Kupoteza mchezo kweli ni jambo gumu ,lakini kumshambulia mchezaji mmoja pekee kwa jambo ambalo ni la timu nzima sio haki. Tunashinda kama timu na tunapoteza kama timu.Alex alijituma sana ,uwanjani kama mchezaji mwingine kwenye kikosi chetu”.

Mpaka sasa Alex Iwobi hajatoa tamko lolote kuhusu shutuma hizo.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Sebastian Coe Eyeing the Top Job in the Olympic Body
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading