HABARI KUU
Rais wa Senegal, Macky Sall, amesema ataondoka madarakani wakati muhula wake utakapotamatika April 2 mwaka huu, hata hivyo akashindwa kutaja tarehe nyingine ya kufanya uchaguzi.
Kauli yake hata hivyo imepokelewa kwa mshangao na wadau wa uchaguzi waliohoji kwanini hajatangaza tarehe nyingine baada ya kuahirisha uchaguzi uliokuwa ufanyike Jumapili ya wiki hii.
Tayari wanasiasa wa upinzani wamekosoa kauli ya Macky Sall, wakijiandaa kwa maandamano zaidi kushinikiza uchaguzi kufanyika kabla ya muhula wake kutamatika.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.