MFAHAMU ABRAHAM MGOWANO MTANZANIA ALIYEFARIKI AKIWA GOOGLE

0

0:00

HABARI KUU

Mwili wa Mtanzania Abraham Mgowano aliyekuwa akiishi na kufanya kazi katika Kampuni ya Google kama Mhandisi wa Programu Endeshi (Software Engineer) umepatikana ukielea katika Mto Miami jijini Florida baada ya kuanguka toka kwenye Boti (Yacht)

Abraham aliripotiwa kupata ajali Februari 24, 2024 akiwa na wenzake 12 pamoja na Kapteni wa Boti hiyo. Polisi walianza kumtafuta kwa kutumia Boti nyingine na Helikopta bila mafanikio hadi walipopata taarifa za kupatikana kwa mwili huo ukielea Februari 27, 2024

Kwa mujibu wa taarifa, Abraham alikuwa Mfanyakazi wa Google kwa miaka 9 baada ya kuwa mmoja wa Wanafunzi bora kutoka Chuo Kikuu cha Stanford. Baadaye aliajiriwa kama Mshauri wa Masuala ya Kompyuta chuoni hapo kwa mwaka mmoja

Aidha, Mtanzania huyo alikuwa kati ya Wanafunzi Bora 12 waliofaulu vizuri Mtihani wa Kidato cha 4 mwaka 2007 ambapo walipata nafasi ya kukutana na kupongezwa na Rais Jakaya Kikwete.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  KURASA ZA MAGAZETI YA HIVI LEO 02/07/2024
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading