NYOTA WA CHELSEA WANAOTARAJIWA KUUZWA

0

0:00

MICHEZO

TREVOH CHALOBAH

Klabu ya Chelsea ina matumaini ya kuwauza baadhi ya mastaa wa kikosi cha kwanza katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.

Nyota hao ni pamoja na beki Trevoh Chalobah mwenye umri wa miaka 24, na Mshambuliaji Armando Broja mwenye umri wa miaka 22.

Mastaa hao wamekuwa wakihusishwa kuondoka tangu dirisha lililopita la majira ya kiangazi kwa sababu hawapati nafasi za kutosha katika kikosi cha kwanza cha matajiri hao wa jiji la London.

Mbali ya mastaa hao pia kuna uwezekano wa kiungo Conor Gallagher mwenye umri wa mika 24 na beki Marc Cucurella mwenye umri wa miaka 25 wakaondoka katika dirisha lijalo.

Kwa upande wa Chalobah amekuwa akihusishwa kutua kwa mabingwa wa Soka nchini Ujerumani Bayern Munich.

Chelsea pia inawauza wachezaji hao, kwa sababu inataka kuboresha timu kwenye dirisha lijalo, ambapo inaonekana kuwa ngumu kusajili kutokana na sheria za matumizi ya kifedha na mwaka jana ilitumia pesa nyingi bila ya kuuza.

Armando Broja
Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Noni Madueke's future at Chelsea is in doubt after the London clubā€™s spending spree - with Newcastle among the clubā€™s ready to offer a loan rescue.
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading