SABABU BILIONEA HARRY ROY VEEVERS KUTOKUZIKWA KWA MIAKA 10

0

0:00

HABARI KUU

MJANE wa marehemu Harry Roy Veevers, raia wa Uingereza aliyekuwa mfanyabiashara mkubwa nchini Kenya na binti zake wawili, wamepinga mahakamani ombi la watoto wengine wa marehemu kuuondoa mwili wa baba yao katika mochwari ya Mombasa ili wakauzike nchini Uingereza.

Parveen Din na binti zake wawili, Hellen Veevers na Alexandra Veevers, wamepinga pia shinikizo la kaka hao wawili ambao mama yao ni mwingine, wanaotaka mahakama iamuru kufanyika upya kwa uchunguzi wa kifo cha baba yao.

Richard John na Philip David Veevers wamekuwa wakitaka mwili wa baba yao ukafanyiwe uchunguzi mara tu utakapowasili Uingereza.

Lakini kupitia kwa wakili Mogaka Omwenga, mjane huyo na binti zake wameshikilia kuwa mahakama ya hakimu mkazi iliendesha kesi ya uchunguzi wa kifo cha tajiri huyo kwa haki.

Veevers alifariki dunia Februari 14, 2013, mjini Mombasa lakini tajiri huyo ambaye hakuacha wosia hajazikwa kutokana na mzozo wa mgawanyo wa mali zake kutokamilika.

Richard na Philip wamekuwa wakishuku kuwa dada zao hao wanaokutana kwa baba, Alexandra na Hellen kwa kushirikiana na mama yao Din, walihusika na kifo cha baba yao. Hata hivyo, uchunguzi uliochukuwa miaka 10 ulihitimisha kuwa, hakuna ushahidi wa kutosha uliowasilishwa mahamkamani kuhusisha mtu yeyote na kifo cha tajiri huyo.

HARRY ROY VEEVERS
Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Why did Chelsea decided to appoint Enzo Maresca as Head Coach
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading