LUVUMBU NZINGA AJIUNGA NA AS VITA CLUB

0:00

MICHEZO

Mchezaji Heritier Luvumbu Nzinga amesaini makataba wa msimu mmoja kwa ajili ya kuitumikia klabu ya AS Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Nyota huyo amesaini mkataba huo mbele ya Rais wa klabu ya AS Vita Club Amadou Diaby.

Hata hivyo, vipengele vya mkataba kati ya mchezaji huyo na mwajiri wake mpya havijawekwa wazi lakini winga huyo amesaini mkataba wa awali wa msimu wa 2024-2025.

Klabu ya AS Vita Club itaanza awamu yake ya mchujo Jumapili ijayo Machi 3 dhidi ya FC les Aigles du Congo ambayo pia imeijiimarisha kwa kuwaleta wachezaji wachache, akiwemo Mukoko Amale.

Kumbuka Luvumbu alirejeshwa nchini baada ya kuwekewa vikwazo na Shirikisho la Soka la Rwanda ambalo lilimkosoa kwa tabia mbaya uwanjani.

Katika ardhi ya Rwanda mnamo Februari 11, Luvumbu alisherehekea bao lake kwa ishara ya kukemea mauaji mashariki mwa DRC sambamba na ukimya wa jumuiya ya Kimataifa.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Polisi wa Argentina wanachunguza vitisho vya kifo vilivyotolewa kwa familia ya mshambuliaji Angel Di Maria nyumbani kwao Roasario.
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading