HIZI NDIZO FAIDA ZA ULAJI WA BAMIA

0:00

MAKALA

Wataalam wa Tiba Mbadala, wanaarifu kwamba ukichukua Bamia na ukaziloweka kwenye maji usiku kucha kisha ukayanywa maji yake basi utapata faida zifuatazo kiafya.

1. Bamia imejaa Virutubisho

Virutubisho hivyo ni muhimu kama vile vitamini A, C, na K, pamoja na madini kama Kalsiamu, Magnesiamu na Potasiamu. Kunywa maji ya bamia hukuruhusu kunyonya kwa urahisi virutubisho hivyo, ambavyo ni muhimu kwa afya bora.

2. Bamia ni nzuri kwa viwango vya Sukari kwenye Damu

Bamia ina nyuzinyuzi ambazo zinaweza kusaidia kupunguza kasi ya ufyonzwaji wa sukari kwenye njia ya usagaji chakula, hivyo kuleta utulivu wa viwango vya sukari kwenye damu.

3. Bamia huboresha Afya ya usagaji Chakula

Ute katika bamia na dutu inayonata inayopatikana katika maganda yake hufanya kazi kama ‘laxative’ asilia na inaweza kusaidia kutuliza na kulainisha njia ya usagaji chakula.

4. Bamia inasaidia kupunguza uzito

Ina kalori chache na nyuzinyuzi nyingi, hivyo kuifanya kuwa nyongeza ya mlo kamili na yenye lishe kwa mlo wowote. Kwa kukuza hisia za kushiba na kupunguza matamanio ya njaa, maji ya bamia yanaweza kusaidia kupunguza uzito.

5. Bamia huongeza kinga

Pia ina wingi wa ‘antioxidants’ ikiwa ni pamoja na vitamini C. Kunywa maji ya bamia kunaweza kusaidia kupunguza hatari ya maambukizi na magonjwa.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  7 BEST ADVICES FROM A FATHER TO A DAUGHTER
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading