DALILI 26 ZINAZOONYESHA KUWA HAUPO TAYARI KUINGIA KWENYE NDOA

0

0:00

MAPENZI

Nani alikwambia wewe ni mtu mzima hata kama una miaka zaidi ya 40 upo tayari kuingia kwenye ndoa? Hizi ndizo dalili za mtu ambaye hayuko tayari kuoa / kuolewa.

  1. Hauna maono kuhusu maisha yako. Hujui unachotaka,jinsi ya kukipata na jinsi ya kuvutia mtu sahihi wa kukusaidia kutimiza maono yako
  2. Hauna hata chanzo kimoja cha kipato. Unapewa tu chakula na kupewa mahitaji mengine.
  3. .Hauna kazi,huna ndoto,huna matamanio, huna maono. Ni mtu upo upo tu.
  4. Wewe ni mtu wa hisia kali/hasira.
  5. Wewe ni mwepesi wa wivu,usiyethamini au kujithamini.
  6. Wewe ni mtu usiye na kiasi. Unaendeshwa na hisia. Unaongea bila mipaka,unatembea bila mipaka. Unalala tu ukiamua,unafanya chochote bila kuwaza au kutafakari.
  7. Wewe ni mtu usiyetii Mamlaka.
  8. Huna mahusiano na MUNGU. Huna muda wa kuhudhuria ibada au kusoma vitabu vya dini.
  9. Huwezi kupika hata chakula na hata kufanya usafi wa nyumba.
  10. Wewe ni mvivu,mtu wa kulala tu,unafanya mambo taratibu na mambo kama haya.
  11. Unachukia Tendo la ndoa
  12. Ni muoga wa tendo la ndoa
  13. Ni mwanaume au Mwanamke mzinifu
  14. Ni Mbaguzi sana ,yaani kuna watu (wanawake/wanaume) hawakufai
  15. Unapenda kusema uongo.
  16. Unapenda kutamba. Husemi ni kipi unapenda na jinsi unavyojisikia.
  17. Wewe ni mtu usiyethubutu
  18. Wewe ni mkatili,mwenye kujipendelea,unayejiona mwenyewe, kiburi,usiye na busara,unayejitenga,mkorofi na mkali.
  19. Hupendi watoto.
  20. Unafuja na kupoteza pesa au huoni thamani ya pesa.
  21. Unapenda kuwa chini (hasa Mwanaume).
  22. Ni mwepesi au dhaifu.
  23. Huna muda kujifunza kuhusu ndoa hata kama unaona vitabu au machapisho.
  24. Una wapenzi wengi.
  25. Unachukia waliopo kwenye Ndoa.
  26. Ni mbinafsi
  27. Ukiwa Mtenda dhambi.
Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading