KAMWE AFUNGUKA SIRI NZITO KUHUSU WACHEZAJI WALIOPATA MAJERAHA YANGA

0:00

MICHEZO

Ofisa habari wa Yanga SC Ally Kamwe amewataka wananchi kutohofia majeraha yanayowakabili wachezaji wao badala yake wajipange kujitokeza Kwa wingi katika mchezo wao wa robo fainal ligi ya mabingwa Afrika mwisho wa mwezi huu dhidi ya Mamelod Sundown.

“Wote tuliona namna wachezaji wetu wawili walivyoshindwa kuendelea na mchezo hapo jana Pacome alilazimika kutoka nje kutokana na maumivu ya goti aliyoyapata dhidi ya Azam na Yao pia alipata maumivu ya paja

Daktari amesema ripoti kamili itatoka baada ya saa 72 Kwa maana ya kesho jioni ndiyo tutajua hali halisi ya wachezaji hao baada ya vipimo kukamilika

Lakini wachezaji wengine ambao wapo majeruhi ni Khalid Aucho naye daktari amesema wiki ijayo ataanza mazoezi ya mpira, Kibwana Shomari na Zawadi Mauya nao wanaendelea na Matibabu

Niwaaambie wananchi mechi dhidi ya Mamelod si mechi ya Pacome Wala mechi ya Aucho ni mechi ya mashabiki hivyo nawaomba mje Kwa wingi tumalize shughuli Benjamin Mkapa kama tulivyofanya dhidi ya CR Belouizdad” Ally Kamwe Meneja wa Habari na mawasiliano Yanga SC.



Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  VARANE NA ERIC TEN HAG NGOMA NZITO MANCHESTER UNITED
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading