KAULI YA GAVANA EMMANUEL TUTUBA YAWAKERA WATANZANIA
HABARI KUU
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutuba amesema hali ya Uchumi ni nzuri na wanaosema Maisha yamekuwa magumu wafanye kazi kwasababu hayajawahi kuwa rahisi tangu Mungu alipoumba Dunia
Amesema
“Kinachotakiwa kila mmoja kufanya kazi. Wengine nimewasikia wakisema Maisha yamekuwa magumu. Kimsingi Maisha hayajawahi kuwa rahisi tangu Mungu alivyoumba Dunia. Alivyomuumba Mwanadamu alisema nenda ukale kwa jasho.”
Ameeleza katika robo 3 za mwaka uliopita, Uchumi ulikua kwa wastani wa 5.2% na matarajio ya takwimu zitakazotoka katika robo ya mwisho, Tanzania inaweza kufikia lengo la ukuaji wa 5.3%
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.