MALAYSIA YAKATAA JUKUMU LA UENYEJI WA MICHEZO YA JUMUIYA YA MADOLA

0

0:00

MICHEZO

Malaysia imekuwa nchi ya pili kulikataa jukumu la uenyeji wa michezo ya Jumuiya ya Madola kwa mwaka 2026.

Hali hii inayaweka mashindano hayo kwenye wasiwasi wa kufutwa kwa mara ya kwanza tangu vita kuu ya Pili ya Dunia.

Nchi hiyo ambayo ilikuwa mwenyeji wa michezo hiyo mwaka 1998 ilikubali kuchukua jukumu baada ya jimbo la Victoria, nchini Australia kuamua kujitoa Julai 2023 kwa sababu za kifedha.

Maafisa nchini humo wamesema Shirikisho la michezo ya Umoja wa Madola(CGF) limetoa fungu la pauni milioni 100 kiasi ambacho hakitoshi.

Naye Msemaji wa Serikali ya Malaysia Fahmi Fadzil amesema “tungekuwa na muda wa kutosha tungeweza kuandaa, lakini muda ni mfupi hivyo hatutoweza”.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Wizkid claims that his fan base, Wizkid FC, resembles a cult-like group.
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading