SERIKALI YAWAITA WAWEKEZAJI KWENYE SGR
HABARI KUU
Shirika la Reli Tanzania (TRC) limechukua hatua muhimu kwa kuwaalika makampuni binafsi kupeleka treni zao kwenye mradi wa Reli ya Kisasa (SGR). Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Bw. Masanja Kadogosa, alitoa tangazo hilo wakati akiongea na wahariri na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali za shirika katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan madarakani.
Bw. Kadogosa alieleza kwamba miundombinu ya reli ya SGR inaruhusu makampuni binafsi kushiriki katika mradi huo, na hii itasaidia kuongeza mapato ya nchi kwa kuhamasisha uwekezaji wa makampuni mbalimbali. Aliongeza kuwa kuna vigezo ambavyo makampuni binafsi vinapaswa kufuata ili kufanya uwekezaji kwenye reli ya SGR.
Aidha, Bw. Kadogosa alisisitiza kuwa mradi wa reli ya kisasa ya SGR utasaidia kuunganisha nchi na hivyo kusisimua uchumi. Wananchi wanaotumia reli walionyesha matumaini yao kuwa treni za kisasa zitasaidia katika shughuli zao za kila siku.
Hadi sasa, mradi huo wa reli ya kisasa ya SGR upo katika hatua mbalimbali za majaribio kabla ya kuanza shughuli rasmi mwezi wa Saba mwaka huu. Hii ni ishara ya jitihada za serikali na wadau katika kuimarisha sekta ya usafirishaji nchini Tanzania. Tutazidi kufuatilia maendeleo ya mradi huu muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.