KAULI YA HARMONIZE KUMFANANISHA MUNGU NA MWANAMKE NI USHETANI

0

0:00

NYOTA WETU

Msanii Harmonize ameingia katika mzozo na waumini wa dini ya Kiislamu huku wakimtaka afute mara moja maneno yake alioandika akimfananisha Mwenyezi Mungu na Mwanamke.

Kwa mujibu wa kile alichoandika kupitia Insta Story yake leo, Msanii huyo anasema imemchukua miaka 30 kugundua ya kuwa pengine Mungu ni Mwanamke kwa asilimia Kubwa.

Mmoja ya waumini wa Dini ya Kiislamu Sheikh Masoud akizungumza amemtaka Harmonize kufuta haraka maandishi hayo akisema Mwenyezi Mungu kwa mujibu wa imani ya dini ya Kiislamu ambayo Harmonize ni muumini wa dini hiyo, hafananishwi na chochote.

ā€œHuu ni msiba mkubwa kwa kijana wetu Harmonizeā€ Anasema Masoud kutoka Altamimy Travel tz moja ya Kampuni ambazo zimekuwa zikipeleka mahujaji Makka.

ā€œAnapaswa afute haraka mno maneno hayaā€ amesema Masoudāœļø

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading