SABABU BENO KAKOLANYA KUIKIMBIA MECHI YA YANGA
MICHEZO
Baada ya klabu ya Singida Big Stars kutoa taarifa kuwa, mlinda mlango wake, Beno Kakolanya ametoroka kambini wakati timu ikikabiliwa na mchezo muhimu dhidi ya Yanga Sc, Beno amekanusha taarifa hizo na kusema kamwe hawezi kutoroka kambini.
Beno Kakolanya ameeleza kuwa hajatoroka kambini bali alitoa taarifa kwa meneja wa timu na kuruhusiwa.
āNilimpa taarifa Meneja kuwa nimepata tatizo na ilikuwa ni siku ya Alhamisi na ilitakiwa niondoke usiku huo huo nikaondoka usiku huo.
āAliyewapa maelekezo anajua ana maana gani waseme hivyo pia niliyempa taarifa naye kafikishaje ujumbe swali lipo hapo.
āIla kwakuwa wamenichafua Sana ngoja wanipe ushahidi nimehujumu wapi timu,ā amesema
Kakolanya.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.