SAKATA LA PAULINE GEKUL LACHUKUA SURA MPYA

0

0:00

HABARI KUU

Mahakama kuu kanda ya Manyara imefutilia mbali rufaa ya Hashimu Ally dhidi ya Mbunge wa jimbo la Babati Mjini Pauline Gekul kwa sababu Rufaa hiyo haikuwa na mashiko mbele ya mahakama hiyo

Maamuzi hayo yametolewa na Jaji wa mahakama kuu kanda ya Manyara Devotha Kamzola huku akiwataka warufani kukata rufaa kama hawajaridhika na maamuzi hayo

Kwa Upande wake wakili wa Hashimu Ally, Peter Madeleka amesema kuwa hajaridhishwa na maamuzi hayo kwani kuna madudu yanaendelea kwenye kesi hiyo hivyo ndani ya siku mbili watahakikisha wanakata rufaa kwenda mahakama ya Rufaa ili haki dhidi ya mteja wake itendeke

Naye wakili wa Pauline Gekul , Efrem Kisanga amesema kuwa maamuzi yaliyotolewa na Jaji Devotha mbele ya mahakama kuu kanda ya Manyara ni maamuzi sahihi hivyo muda wowote kuanzia sasa mteja wake atafungua kesi ya maadai kwa wale wote waliomchafĆŗa kupitia Kashfa hiyo na ukweli wote utajulikana ndani ya musa mfupi

Ikumbukwe Kuwa Pauline Gekul Ơlifikishwa mahakama ya wilaya ya Babati kwa Kesi ya kumuingizia chupa Ʊyuma ya maumbile aliyekua mfanyakazi wake Hashimu Ally na kesi hiyo kutupitiliwa mbali na Mkurugenzi wa Mashtaka kutokana na mamlaka aliyopewa

Hii ni Mara ya Pili Pauline Gekul kushinda kesi hiyi licha ya mrufani wake kutaka kukata rufaa kwenye mahakama ya rufaa

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading