Tomas Tuchel akanusha tetesi za kuombwa kusalia Bayern Munich

0:00

MICHEZO

“Imekuwa bahati kuwa hapa, lakini lazima niseme ukweli, kwa sababu tuna makubaliano, hakuna sababu ya kutilia shaka makubaliano haya kwa sasa. Tumefika hapa kwa kushirikiana na Uongozi pamoja na Wachezaji, lakini sina budi kuondoka mwishoni mwa msimu huu.

“Sihitaji kulazimishwa kuendelea kuwa hapa, wala mimi sitalazimisha kuwa hapa, kilichobaki kwangu kwa sasa ni kuhakikisha naiacha klabu katika mazingira mazuri, tupo kwenye michuano mikubwa Barani Ulaya, nitahakikisha tunapambana ili tuingie Fainali na ikiwezekana kutwaa Ubingwa wa Ulaya.

“Wapinzani wangu (Real Madrid) wapo vizuri hasa wapokuwa katika hatua kama hii tunayokwenda kukutana nao, lakini mchezo bado upo wazi kila mmoja anaweza kushinda na kusonga mbele.”

Swali lingine aliloulizwa Tuchel ni kama ataweza kurejea Chelsea, lakini alijibu: “Nisingependa kujibu lakini sio siri kwamba niliipenda Chelsea, niliipenda Uingereza na niliipenda Ligi ya EPL kwa hakika, ulikuwa wakati wa kipekee sana na ninaukumbuka vizuri sana.” amesema Tuchel

Iwapo Bayern watashinda dhidi ya Real Madrid na kutinga hatua ya Fainali itakayochezwa katika Uwanja wa Wembley, Tuchel atakuwa meneja wa pili kuzipeleka timu tatu tofauti katika Fainali ya UEFA Champions League.

Loading

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV

Related News 📫

Old tweet of Davido speaking on Tonto...
CELEBRITIES An old tweet of Davido speaking of Tonto Dikeh’s...
Read more
CHANZO KIKUU CHA TATIZO LA HARUFU MBAYA...
HARI YA ACID YA UKE (VAGINA PH)PH ni kipimo cha...
Read more
Liverpool back in groove, Chelsea thrash West...
LONDON, - Liverpool returned to winning ways in the Premier...
Read more
TONALI AFUNGIWA MIEZI 10 KISA KUBET ...
MICHEZO
See also  ARSENAL WAPO KILELENI MWA MSIMAMO WA LIGI YA EPL
Kiungo wa Newcastle United, Sandro Tonali amefungiwa miezi 10...
Read more

Leave a Reply