Manchester United na Bayern Munich zaingia vitani

0:00

MICHEZO

Saa chache baada ya Klabu ya Chelsea kutangaza kuachana na Mauricio Pochettino, Klabu za Manchester United na Bayern Munich zimeanza kuhusishwa na mpango wa kumuajiri Kocha huyo kutoka nchini Argentina.

Chelsea imetangaza kusitisha Mkataba wa miaka miwili wa Kocha huyo, baada ya kufanya mazungumzo kwa kina na pande zote mbili kukubaliana kuvunjwa kwa Mkataba huo, ambapo hatua hiyo inamfanya Mauricio Pochettino kuwa huru kwa sasa.

Kwa sasa Manchester United wapo kwenye shinikizo la kumwacha Kocha Erik ten Hag, huku asilimi ndogo ya viongozi wakipendekeza Kocha huyo aachwe klabuni hapo kwa msimu mwingine.

Upande wa Bayern Munich wapo kwenye mpango wa kumsaka mbadala wa Kocha Thomas Tuchel ambaye anajiandaa kuondoka klabuni hapo baada ya kumaliza msimu wa 2023/24.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Obrey Chirwa afunguka mazito na mipango ya kulipiza kisasi
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading