NANI KUWA MFUNGAJI KATI YA AZIZ KI NA FEISAL SALUM?

0

0:00

Leo jioni tutajua nani Mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu huu, Mchuano uko kwa nyota wawili Stephane Aziz KI wa Yanga SC na Feisal Salum wa Azam FC. Mchuano sio mdogo. Kila mmoja ameshafunga mabao 18.

Yanga SC watakuwa katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi kucheza dhidi ya Tanzania Prisons kutoka Mbeya.

Mchezo huu utafuatiliwa kwa sababu moja tu. Kwa sababu ya Aziz KI. Yanga SC watatamani kuona Aziz KI anafunga mabao katika pambano hili la mwisho.

Mchezo mwingine utamhumusisha Feisal na Azam FC yake. Mchezo huu utachezwa katika Uwanja wa Nyankumbu Jijini Geita.

Azam FC watataka mambo mawili katika pambano hili. Mosi kushinda ili kuyaweka hai matumaini ya kucheza Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika. Lakini pili ni kutamani kuona Feisal anafunga mabao katika pambano hilo.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  British number one Jack Draper says he had a "difficult" time after his integrity was questioned following last week's Cincinnati Open.
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading