JOSEPH MBILINYI “SUGU” AMBWAGA PETER MSIGWA

0

0:00

Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu Sugu ametangazwa Mshindi kwenye uchaguzi wa kumtafuta Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa ambapo amemuangusha aliyekuwa anatetea kiti hicho, Mchungaji Peter Msigwa.

Matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika leo May 29,2024 katika Mji wa Makambako Mkoani Njombe yametangazwa usiku huu baada ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa kupiga kura.

Sugu ameshinda kwa asilimia 51 huku Mchungaji Msigwa akipata asilimia 49 ya kura zilizopigwa.

Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Mshindi ni Frank Mwakajoka ambaye ni Mbunge wa zamani wa Tunduma.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Shooting at Donald Trump Rally
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading