WIMBI LA JOTO KALI INDIA LAUA WATU

0

0:00

Mji Mkuu wa India New Delhi, unakabiliwa na wimbi la joto kali hali iliyovunja rekodi hadi kufikia nyuzijoto 52.3C ( 126.1F).

Joto hilo limekuwa likisababisha Wanafunzi Mashariki mwa nchi hiyo kupoteza fahamu na watu kadhaa kupoteza maisha katika jimbo la Rajasthan.

Kwa mujibu wa muuguzi mmoja, joto hilo limesababisha miili ya wengi kuishiwa maji hivyo kupelekea hali za kuzimia, kutapika na kujisikia kizunguzungu.

India pamoja na sehemu za Asia ya Kusini na Asia ya Kusini Mashariki zimekuwa zikikabiliwa na joto kali tangu mwezi uliopita.

Utabiri wa hali ya hewa unaonyesha kuwa hali hiyo itaanza kupoa kuanzia Alhamisi.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Kiongozi wa upinzani Nchini Israel Yair Lapid ametoa wito kwa Waziri Mkuu wa taifa hilo Benjamin Netanyahu, kuzingatia mpango uliotangazwa na rais wa Marekani Joe Biden wa kusitisha mapigano Gaza.
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading