Kwanini Biden amekiri kuzidiwa na Donald Trump?
Rais wa Marekani Joe Biden kwa mara nyingine, amekiri kuwa hakuonesha uimara wakati wa mdahalo wa Televisheni dhidi ya mpinzani wake, rais wa zamani Donald Trump rump wiki iliyopita, na kuapa kujiimarisha katika siku zijazo na katika uwanja wa kampeni kuelekea uchaguzi wa mwezi Novemba.
Siku ya Jumatano, Biden alikutana na kufanya mazungumzo na Magavana wa chama chake cha Demokratic ambao wamesema wanamuunga mkono mpaka mwisho.
Kumekuwa na ripoti kuwa Biden mwenye umri wa miaka 81, huenda akaachana na harakati za kutafuta urais kwa muhula wa pili, huku Ikulu ya white house ikisema hakuna mpango huo.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.