DiscoverCars.com   
                                                                   
6 / 100 SEO Score

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imebaini ukiukwaji wa sheria na taratibu kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda kuhusu amri aliyoitoa kukamatwa mkazi wa mkoa huo hivi karibuni.

Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu ameeleza hayo kwa waandishi wa habari mkoani Dodoma leo wakati akisoma taarifa ua chunguzi mbalimbali zilizofanywa na tume hiyo.

Katika uchunguzi iliyoufanya tume hiyo kuhusu Mkuu huyo wa mkoa iliyohusu tuhuma dhidi yake ya kutoa amri kukamatwa na kuwekwa mahabusu mkazi wa Mkoa wa Arusha kinyume na utaratibu wa kisheria mnamo Juni 2024, tume imebaini kuwa amri iliyotolewa na Mkuu huyo ya kumkamata na kumuweka ndani mkazi huyo haikuwa halali na haikuzingatia aina ya makossa na utaratibu ulioainishwa kisheria wa utekelezaji wa mamlaka hay.

Katika hatua nyingine Tume ilichunguza malalamiko dhidi ya Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul na wenzake kudaiwa kuwafanyia vitendo vya ukatili na udhalilishaji Hashim Ally na Michael Isaria kwa kuwaingiza chupa sehemu ya haja kubwa ambapo uchunguzi wa tume haukubaini suala hilo kufanyika.

Awali Tume ililazimika kufanyia uchunguzi maalumu malalamiko 22 yakiwemo masuala ya ardhi, uharibifu wa mazingira, tuhuma za vitendo vya ukatili katika vizuizi na matumizi mabaya ya madaraka ambayo yaliwahusu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, Mbunge wa Bababati Mjini, Pauline Gekul na tuhuma mbalimbali za askari polisi dhidi ya kuwakamata wananchi kinyume na utaratibu na sheria katika maeneo mbalimbali.

Masuala mengine yaliyofanyiwa uchunguzi na tume hiyo ni pamoja na malalamiko dhidi ya Mgodi wa North Mara kudaiwa kutozingatia utaratibu wa utwaaji wa ardhi ya wananchi ambayo hata hivyo tume haikubaini suala hilo, suala la Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kutwaa ardhi ya Kijiji cha Ludewa ambalo pia tume haikubaini suala hilo kwa kushindwa kuthibitisha madai ya wananchi hao.

1 total views , 1 views today

Love it or Not? Let us know!

Rate this

Login to submit a rating.
0.0
0 reviews
5
(0)
4
(0)
3
(0)
2
(0)
1
(0)

    Related News 📫

    Cristiano Ronaldo etched his name in the...
    In a groundbreaking achievement, football legend Cristiano Ronaldo has etched...
    Juventus lose ground in title race after...
    TURIN, Italy, 🇮🇹 - Juventus twice came from behind to...
    Caicedo's strike ruins Man United's celebrations in...
    MANCHESTER, England, 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 - Moises Caicedo's blistering second-half strike cancelled...
    See also  Girona coach laments lack of depth after Real Sociedad loss

    Leave a Reply

                     
                                                                                                                                                                                                           

    Get 30% off your first purchase

    X
    Open chat
    Hello
    Can we help you?
    Privacy Overview

    This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.