DiscoverCars.com   
                                                                   
4 / 100 SEO Score

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo ,John Heche amesema ukimya wake yeye binafsi na wenzake (waliokaa kimya) ndani ya chama hicho unatokana na kile alichokieleza ni kuepusha mpasuko zaidi ndani ya chama hicho hususani katika kipindi hiki ambacho chama hicho kipo kwenye mchakato wa ndani wa uchaguzi

Kupitia chapisho lake aliloweka kwenye mitandao yake binafsi ya kijamii Heche amesema kama Taifa kwa ujumla tunalo jukumu la msingi la kuhakikisha nchi inapata chama mbadala na serikali mbadala itakayokuwa na wajibu wa msingi wa kuwatumikia watu na kuwaondoa Watanzania katika dimbwi la umaskini uliodumi kwa takribani miaka 63 ya uhuru

Amesema Watanzania wana shauku ya kuona serikali na chama cha siasa kitakachopinga rushwa kwa vitendo na bila aibu, chama cha siasa kinachochukia umaskini, kitakachoongoza na kutumia raslimali za Taifa kwa kuendeleza maisha ya Watanzania na si vinginevyo

“Hata hivyo katika wakati muafaka na muda sio mrefu nitazungumza na kutoa muelekeo wangu katika jambo hili kubwa” -Heche

Hata hivyo, Heche ambaye pia ni Mbunge wa zamani wa jimbo la Tarime vijijini kupitia CHADEMA amesema amepokea jumbe nyingi kwa njia tofauti ikiwemo simu kuhusiana na ukimya wake huku wengi wanaomtafuta wakimuomba aseme jambo kuhusiana na kile kinachoendelea katika chama hicho

“Nimepata jumbe nyingi, simu nyingi, nawahakikishia Watanzania na wanachama wa CHADEMA kwamba nimewasikia na nitazungumza” -Heche

Ikumbukwe, miongoni mwa jumbe na mijadala iliyoko sana kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa (inayomuhusu John Heche) ni ile inayomuomba kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tanzania Bara.

See also  England manager Tuchel vows to earn right to sing anthem

Loading

Love it or Not? Let us know!

Rate this

Login to submit a rating.
0.0
0 reviews
5
(0)
4
(0)
3
(0)
2
(0)
1
(0)

    Leave a Reply

                     
                                                                                                                                                                                                           

    Get 30% off your first purchase

    X
    Open chat
    Hello
    Can we help you?
    Privacy Overview

    This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.