FISTON MAYELE AFUNGUKA MAZITO BAADA YA KUONDOKA TANZANIA
NYOTA WETU
Mshambuliaji wa Pyramids FC ya Misri, Fiston Mayele akifanya mahojiano na kituo cha habari cha Azam, ameeleza kuwa kocha aliyemkuta ndani ya kikosi cha Pyramids wakati anatokea Yanga Sc alitaka kumtoa kwa mkopo Disemba 2023 lakini Rais wa Klabu hiyo alizuia jambo hilo na kumuondosha kocha huyo.
āWakati nakuja Pyramids kocha niliyemkuta alikuwa na wachezaji wake, na mimi nikaingia kuna wakati alinichezesha nilikuwa natoa assist au nafunga najua mechi hii nimefanya vizuri hivyo mechi ijayo nitaanza, mechi inakuja ananiweka tena nje.
āUlifika wakati nikaenda kuongea na viongozi wa timu nikawaambia sikuja Pyramids kukaa nje kama mnaona mnaniweka nje Disemba (Disemba 2023) naondoka, niliwaambia hapa nimekuja kucheza.
āDisemba tulienda kucheza Kombe la Uarabuni na tukafungwa, baada ya ile mechi yule kocha akaandika list ya wachezaji wakutolewa kwa Mkopo jina langu lilikuwa la kwanza kwenye list, Rais wa timu akamwambia sawa tutakujibu.
āMimi nikiwa AFCON yule Rais akanipigia akaniambia jina lako limetolewa huku utolewe kwa mkopo lakini siwezi kukubali kwasababu naamini utaisaidia timu yangu akaniambia mimi nitamuondoa yeye (Kocha), Rais akamuondoa yule kocha,ā Mayele.
Fiston Mayele amesema pia baada ya Pyramids kumtambulisha kama mchezaji wao mpya kesho yake aliamka na kukuta mguu wake umevimba hivyo alifunga safari kurejea Tanzania hadi kwa Nabii, Boniface Mwamposa kufanyiwa maombi.
āBaada ya ile mechi ya dodoma nililia sana niliumia mguu ulivimba hata kutembea sikuweza, hospitali walisema nimevunjika lakini hawawezi kuniweka hogo maana mguu umevimba utaoza alafu watanikata hivyo natakiwa nikae tuu hadi mguu upungue, nikaanza kuwaza vitu vingi nikasafiri kwenda Congo.
āNilivyoenda Congo Mungu akasaidia nikawa sawa nikaenda Pyramids kusaini walivyonitambulisha kesho yake nikaamka mguu umevimba tena nikasema hapana, nikarudi tena Congo Kisha Tanzania nikaenda kwa Mwamposa akanisaidia mguu ukarudi kidogo.
āMpaka Leo mguu wangu mmoja umevimba haujarudi kama zamani, hakuna maumivu Lakini mguu mmoja ni mkubwa kuliko mwingine,ā Mayele.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.