GABRIEL AMPIGIA CHAPUO SALIBA

0:00

MICHEZO

Beki kutoka nchini Brazil na Klabu ya Arsenal Gabriel dos Santos Magalhães, amesema kuna mambo makubwa yanakuja kwa The Gunners ikiwa wanaweza kumaliza msimu huu kwa kushinda michezo yao yote iliyosalia, huku akijadili jinsi safu ya ulinzi ya klabu hiyo ilivyoimarika.

Kabla ya mpambano wao mkali wa London daby dhidi ya Chelsea utakaopigwa baadae leo Jumanne (Aprili 23), Kikosi cha wa Mikel Arteta kipo kileleni mwa msimamo wa Ligi ya England kikiwa na alama 74 sawa na Liverpool, huku Manchester City ikiwa na alama 73 na mchezo mmoja mkononi.

Arsenal wanaingia katika hatua ya mwisho msimu huu wakiwa na matumaini ya kupata mwenendo mzuri wa matokeo, jambo ambalo halikuwa hivyo msimu uliopita, kwani Beki William Saliba aliumia wakati wa mchezo wa Ligi ya Barani Ulaya ‘UEFA Europa League’ dhidi ya Sporting Lisbon ya Ureno, mnamo Machi 16 mwaka jana.

Beki huyo kutoka nchini Ufaransa hakuonekana tena kwenye Michezo ya Ligi Kuu, hali ambayo ilipunguza ukali wa safu ya Ulinzi ya Arsenal na kuipa nafasi Man City kutwaa taji lao la tano ndani ya miaka sita.

Kutokana na utofauti wa msimu uliopita na msimu huu, Beki Gabriel amesema ni hatua nzuri kwa Arsenal kuendelea kuwa na Beki kama Saliba hadi sasa, kwani anaamini uwepo wake umeongeza kitu kwenye kikosi chao ambacho msimu huu kinapambana kurudisha heshima ya ubingwa iliyopotea miaka 20 iliyoipita.

Gabriel amesema: “Ilikuwa ngumu kwetu kwa sababu tulikuwa tunacheza kila mechi pamoja, na bila shaka mambo hubadilika wachezaji wengine wanapoingia.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  SIMBA YAKUBALI KICHAPO MBELE YA AL AHLY

Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading