Borussia Dortmund yatinga Fainali kibabe ikiichapa PSG

0:00

MICHEZO

Mlinzi wa kati Mats Hummels alifunga bao pekee kwa Borussia Dortmund na kuwapa tiketi ya kucheza fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya na kuwaondosha PSG kwa matokeo ya jumla ya 2-0 baada ya mchezo wa kwanza kushinda pia 1-0 walipokuwa nyumbani Signal Iduna Park.

Mara ya mwisho kwa Dortmund kutinga fainali ya michuano hiyo ilikuwa ni miaka 11 iliyopita walipopoteza dhidi ya Bayern Munich kwenye fainali iliyopigwa kwenye dimba la Wembley na sasa wanarejea kujiuliza tena kwenye dimba hilo wakimsubiri mshindi kati ya Real Madrid na Bayern Munich

Beki Mats Hummels na Marco Reus ndiye wachezaji pekee waliokuwepo kwenye kikosi cha Dortmund mara ya mwisho walipocheza fainali ya UCL kwenye uwanja wa Wembley

PSG sasa watalazimika kusubiri kwa msimu mwingine kujaribu tena bahati yao kwenye ligi ya mabingwa Ulaya baada ya mwaka huu kuendeleza jinamizi la kukosa bahati kwani wameacha rekodi ya kuwa timu ambayo mashuti yao yamegonga mwamba mara nyingi zaidi wakifanya hivyo mara 13 msimu huu pekee


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  WATU SITA WAKAMATWA MAUAJI YA RAPA A.K.A
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading