CHAD YAMPATA RAIS MPYA WA MPITO

0:00

HABARI KUU

Kwa mujibu wa matokeo ya awali ya Tume ya Uchaguzi, Rais wa mpito wa Chad, Mahamat Idriss Déby Itno, ameshinda uchaguzi wa Urais wa Mei 6 kwa asilimia 61.03 ya kura, mbele ya mpinzani wake mkuu, Waziri Mkuu Succès Masra, aliyepata kura 18.53%.

Hata hivyo Bw.Masra amedai kushinda uchaguzi huo katika raundi ya kwanza.

Waziri Mkuu wa zamani Albert Pahimi Padacé amekamata nafasi ya tatu akipata kura 16.91% kiwango cha walioshiriki uchaguzi ikiwa ni 75.89%, kulingana na tume ya uchaguzi.

Matokeo ya muda ya uchaguzi wa urais wa Jumatatu nchini Chad yalitangazwa na Kiongozi wa Tume ya Uchaguzi Alhamisi jioni, Mei 9, siku 12 kabla ya tarehe iliyopangwa ambapo matokeo hayo yanatarajia kuthibitishwa na Baraza la Katiba nchini humo kama matokeo rasmi.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Ancelotti lauds 'rare and extraordinary' Vinicius after win against Dortmund
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading