Historia ya Mwanamziki Diamond platnumz

0

0:00


Nasibu Abdul Juma Isaac (maarufu kwa jina la kisanii kama Diamond Platnumz; majina mengine ya kisanii ni kama Chibu, Simba, Nasibu kichwa, Simba la masimba ama Dangote; alizaliwa Dar es Salaam, Tanzania, 2 Oktoba 1989) ni mwimbaji wa nyimbo za Bongo Fleva na dansa kutoka nchini Tanzania. Ni mwimbaji na mtunzi wa muziki wa Kitanzania ambaye ana uwezo mkubwa wa kiushindani zaidi ya wasanii wa mataifa mengine. Hivyo ana mashabiki wengi ndani na nje ya Tanzania. Inasemekana kuwa ndiye msanii wa Mashariki na Kati mwa Afrika anayependwa sana na kupambwa na watu wengi kwa sasa.

Mzaliwa wa Dar es Salaam mwenye asili ya Kigoma, Diamond ni Mwislamu.

Mwaka 2010, alikubali chama tawala cha Tanzania, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mgombea wake wa urais, Jakaya Kikwete. Pia aliandika remix ya wimbo wake mmoja.

Nasibu Juma anasimamiwa na Babu Tale pamoja na Said Fella kutoka sekta ya muziki wa Tanzania. Anasemekana kuwa mwanamuziki tajiri zaidi katika Afrika Mashariki. Mnamo Februari 2018 alizindua Wasafi Tv na redio yake mpya nchini Tanzania. Ni mwanamuziki wa pili baada ya Youssou Ndour wa Senegal kumiliki TV na kituo cha redio katika Afrika.

Pia alizindua albamu yake ya kwanza A Boy From Tandale huko Nairobi katika maandamano ya 2018.

Ana watoto wanne ambao ni Dylan Abdul (aliyezaa na Hamisa Mobeto japo kumekuwa na sintofahamu juu ya Diamond kuwa baba wa mtoto huyo), Lattifah na Nillan Nasibu Abdul (aliyezaa na Zari Hassan, mfanyabiashara wa Uganda) pamoja na Nasibu Abdul Nasibu (aliyemzaa na mtangazaji na mwanamuziki Natasha Donna toka Kenya). Pia ni rafiki wa wengi.

See also  Napoli still expect to complete a £12.5million deal for Billy Gilmour this week despite pressing ahead with signing compatriot Scott McTominay.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading