Michezo
Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa stars” imeandika rekodi nyingine ya kufuzu kucheza michuano ya Afrika kwa mara ya tatu baada ya kuilazimisha sare ya timu ya ALGERIA ya 0-0 .
Tanzania ambayo ilishiriki AFRICON kwa mara ya kwanza mwaka 1980 na baadaye 2019.imekamilisha michezo yake ya Kundi F kwa kukusanya jumla ya alama 8 nyuma ya ALGERIA mwenye alama 16 na mbele ya Uganda mwenye alama 7 na Niger aliyeshika mkia kwa alama 2.
Michuano ya AFRICON inatarajiwa kufanyika January 13 hadi February 11,2024 katika nchi ya Ivory Coast.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.