CRISTIANO RONALDO AMCHEKA MESSI

0:00

MICHEZO

Cristiano Ronaldo achekeshwa na maneno ya Mwandishi wa habari aliyekuwa akizungumzia tuzo za Ballon d’Or ya nane ya Mshambuliaji Lionel Messi na kuutafsiri kama “upendeleo “.

Ronaldo aliweka comment yake hiyo kwenye mtandao wa As Television uliomuonyesha mwanahabari Tomas Roncero ,akisema kuwa

“Habari, tulichodhani kuwa wanaenda kumpa Ballon dOr nyingine Messi, kimetokea.

Alishinda kombe la Dunia, ndio,lakini kwa penati 6. Kombe la Dunia lilikuwa miezi 10 iliopita .na sasa tuko Novemba. Messi ana Ballon d’Or nane ,lakini anapaswa kuwa nazo tano . Ana Ballon dOr ya Iniesta na Xavi,Robert Lewandowski ambaye alishinda mataji sita katika msimu mmoja na Haaland ambaye amekuwa mfungaji bora kwa kila ligi anayoshiriki”

Ronaldo ali-like chapisho hilo lenye utata ,na kuacha comment ya emoji nne za kucheka .

Comment hiyo ya Mshambuliaji wa Al-Nassr ina zaidi ya like 90,000.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  DIAMOND SASA APIGWA CHINI YOUTUBE
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading