MICHEZO
Mashabiki 11 wa soka wamejeruhiwa baada ya fataki kurushwa wakati wa mechi ya Bundesliga kati ya timu za Augsburg na Hoffenheim jana.
Kwa mujibu wa polisi ,fataki hiyo ilirushwa kutokea upande wa uwanja wa WWK Arena . Kelele kubwa ilisikika uwanjani humo huku watu kadhaa wakijeruhiwa wakati wa mlipuko.
Mchezo ulisimamishwa wakati huduma za dharura zikitolewa na baadaye uliendelea na kutoka kwa sare ya 1-1.
Polisi wameanza uchunguzi kuhusiana na tukio hilo na washukiwa wawili washakamatwa.
Discover more from JUNIITV.ONLINE
Subscribe to get the latest posts sent to your email.