Kocha wa FC Porto, Sergio Conceicao amemshutumu Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta kwa kuitukana familia yake wakati Waingereza hao juzi Jumanne (Machi 12) usiku wakishinda kwa mikwaju ya Penati dhidi ya timu hiyo ya Ureno na kujikatia tiketi ya kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza tangu 2010.

0

0:00

Alipotakiwa kufafanua kilichotokea, Conceicao kupitia mkalimani wa Shirikisho la Soka Barani Ulaya ‘UEFA’ alinukuliwa akisema, “Wakati wa mchezo na kuelekea benchi yeye, kwa Kihispania, sijui ndio ilivyo kwa makocha wa Hispania, aliitukana familia yangu.

“Na kisha mwishoni, nilisema tafadhali usimtukane mtu ambaye hayupo hapa kati yetu, unapaswa kuzingatia mafunzo ya timu yako,” alisema Conceicao.

Hata hivyo, vyanzo vya Arsenal viliambia ESPN kwamba Arteta alikanusha vikali shutuma hizo.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  HUU NDIO MKATABA MPYA WA JONAS MKUDE NDANI YA YOUNG AFRICANS
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading