MFAHAMU BALOZI ALI IDI SIWA MKURUGENZI MPYA USALAMA WA TAIFA

0:00

Makala Fupi

Jana Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Mkurugenzi mpya wa usalama wa Taifa na safari hii ni Balozi Ali Idi Siwa . Hii inakuja katika miaka 2 ya uongozi wa Rais Samia Suluhu kuwa na teuzi za Wakurugenzi watatu ndani ya muda mfupi. Wakati Rais Samia Suluhu anaingia madarakani kufuatia,kifo cha mtangulizi wake John Pombe Magufuli alikuwepo Diwani Athumani Msuya kabla ya kumteuwa Said Hussein Masoro January 2023 mpaka Agosti 23.

Balozi Ali Idi Siwa

Uzoefu wa Balozi Ali Idi Siwa

—- Alianza utumishi mwaka 1977

—- 2001-2014 Alikuwa Afisa Mkuu Mambo ya Nje katika Balozi za Abu Dhabi, Urusi na Ujerumani.

— Agosti 2014-2018 aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda.

Septemba 2018 aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF.

Baada ya kumtazama Balozi Ali Idi Siwa, ifuatayo ni orodha ya Wakurugenzi wapya wa Idara ya Taifa;.

Emilio Mzena (1961-1975)

Lawrence Gama (1975-1978)

Dkt Hassy Kitine (1978-1980)

Dkt Augustine Mahiga (1980-1983)

Luteni Jenerali Imran Kombe (1983-1995). Huyu aliuwawa na polisi Juni 30,1996.

Kanali Apson Mwang’onda (1995-2005)

OTHMAN RASHID (2005-2016)

Dkt Modestus Kapilimba (2016-2019)

Diwani Athumani Msuya (2019-2023)

Said Hussein Masoro January 2023-agost 2023.

Mkuu huyu wa Usalama anakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha Katiba Mpya inapatikana na suala la Uwekezaji wa Emirates Dubai kwenye Bandari za Tanzania unafikia kwenye mwisho mzuri ambako kwasasa kama umekwama.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  RAIS WA VIETNAM AJIUZULU KWA KUSHINDWA KUPAMBANA NA UFISADI
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading