MISRI NA MAREKANI ZAKUBALI KUFUNGUA MIPAKA

0

0:00

HABARI KUU.

Rais Joe Biden wa Marekani na Abdel Fattah al-Sisi wa Misri wamekubali kufungua kivuko cha Rafah ili kuruhusu hadi lori 20 za misaada kuingia Gaza.

“Rais wa Misri Abdel Fattah al-sisi na Rais wa Marekani Joe Biden wamekubaliana juu ya utoaji endelevu wa misaada ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza kupitia kituo cha Rafah”.

Alisema msemaji wa Rais Ahmedy Fahmy katika taarifa yake.

Mazungumzo kati ya viongozi hao wawili yalisema msaada huo unaratibiwa na mamlaka husika katika nchi hizo zenye makundi ya kimataifa ya kibinadamu, chini ya umoja wa Mataifa.

Usafirishaji huo labda hautapita Ijumaa, Biden alisema, akitoa mfano wa ukarabati wa barabara.

“Watatengeneza barabara, wanapaswa kujaza mashimo ili kupata lori ziweze kupita.Na hilo litafanyika- wanatarajia itachukuwa takribani saa nane (Alhamisi) . Kwahiyo kunaweza kuwa hakuna kitu kinachoendelea hadi…pengine hadi ijumaa”.

Aliwaambia wanahabari siku ya jumatano.

Aliongeza kuwa lori hizo 20 ziliwakilisha “hatua ya kwanza ” lakini akasema “lori 150 hivi” kwa jumla zilikuwa zikisubiri. Ikiwa wale waliruhusiwa kuvuka au la itategemea “jinsi itakavyokuwa”.

Mashirika ya kimataifa yanasema hitaji la misaada ni jambo la dharura.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  BURUNDI NA RWANDA ZAINGIA KWENYE VITA YA KIUCHUMI
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading