0:00

MICHEZO

Mshambuliaji wa Paris St-Germain Kylian Mbappe amefikia makubaliano ya kujiunga na Real Madrid msimu mpya utakapoanza.

Nahodha huyu wa Ufaransa, 25, aliwaambia PSG kuwa ana nia ya kuondoka, mkataba wake utakapomalizika mwezi Juni 2024.

Mbappe hajasaini mkataba na Real Madrid bado, lakini mkataba huo huenda ukatangazwa mara tu itakapobainika kuwa Real na PSG haziwezi kukutana kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.

Mbappe, mshindi wa Kombe la Dunia, ndio mfugaji bora wa PSG akiwa na magoli 244.

Mbappe alitaka kumaliza suala la hatma yake kabla ya mwezi Machi, na Februari 13, kabla ya kuanza mazoezi alikutana na Rais wa PSG Nasser Al-Khelaifi na kumwambia kuwa anaondoka na atajiunga na Real.

Kufuatia taarifa za kuondoka kwake Alhamisi iliyopita, Mbappe hakuanza mchezo dhidi ya Nantes wa Jumamosi, lakini aliingia baadaye na kufunga bao pekee kwa mkwaju wa penati na kuifanya PSG kuongoza ligi ya Ufaransa kwa tofauti ya pointi 14.

Anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano na Real, na kulipwa Euro milioni 15 kwa mwaka,(Tshs 41,288,553,000B) pamoja na Euro milioni 150 kama marupurupu ya kusaini, ambazo zitalipwa kwa kipindi cha miaka mitano.

Iwapo Luka Modric ataondoka Real, Mbappe atarithi jezi namba 10, ambayo huivaa akiwa na timu ya taifa ya Ufaransa.


Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading