Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amekiri kuwa chama chake cha African National Congress (ANC) kimepata changamoto katika matokeo ya uchaguzi, baada ya chama hicho kupoteza wingi wa kura kwa mara ya kwanza tangu utawala wa kibaguzi kumalizika miaka 30 iliyopita.

0

0:00

Chama cha ANC, ambacho kiliwahi kuongozwa na Nelson Mandela, kilishinda viti 159 katika bunge lenye viti 400 katika uchaguzi wa Jumatano, idadi ya chini kutoka 230 katika bunge lililopita.

Ramaphosa bado alitaja matokeo kama ushindi kwa demokrasia, akitoa wito kwa vyama vinavyopingana kutafuta muafaka na kujiandaa kwa mazungumzo ya muungano.

Chama cha upinzani cha Democratic Alliance (DA) kimesema kiko tayari kwa mazungumzo ya muungano na Bw Ramaphosa, lakini kinapinga vipaumbele vingi vya serikali yake.

Pamoja na kura zote kuhesabiwa, ANC ilimaliza kwa kupata 40% chini kutoka 58% katika matokeo ya uchaguzi uliopita, ambayo yalitangazwa siku ya Jumapili.

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  Jamaican sprint icon Shelly-Ann Fraser-Pryce withdrew from the Olympic 100m competition before her semi-final at Paris 2024 on Saturday.
Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading