KAMA UNATAKA KUUTEKA MOYO WA MUMEO UWE RAFIKI YAKE WA KWELI KWA MAMBO HAYA.

0

0:00

Ili kutengeneza au kuimarisha urafiki katika ndoa, jaribu kufanya yafuatayo:

  1. Sikiliza, sikiliza, msikilize: Jitahidi sana kusikiliza bila kukengeushwa, bila kutengeneza orodha ndefu ya mambo akilini mwako wakati anapoongea na bila kushughulishwa na chochote. Kumbuka anachokushirikisha kuhusu kazi, malengo yake, n.k.
  2. Zungumza naye mambo ya siku hiyo, muunge mkono na tengeneza mazingira ya maelewano.
  3. Angalia vipengele anavyovipenda, visome na ujiandae kuvizungumzia.
  4. Daima sema “TAFADHALI” na “AHSANTE”, hata kama ndoa yenu ina muda mrefu.
  5. Kuleni pamoja angalau mara moja kwa siku.
  6. Uwe msamehevu: Usitazame sana kasoro zake na jifunze kukumbuka sifa zake nzuri. Kila mtu anazo sifa hizo… hivyo weka macho na akili yako kwenye sifa hizo chanya.
  7. Panga shughuli za pamoja, kama vile kusafiri pamoja, kutembea pamoja, kula pamoja, kwenda nje pamoja… chochote ambacho mtakifurahia mkiwa pamoja.
  8. Chekeni pamoja: Usiufanye uhusiano wako na mumeo kuwa mkavu sana usiokuwa na hata maskhara na mzaha. Wanandoa wanaoweza kucheka pamoja, hudumu pamoja.
  9. Wekeni muda wa kujongeleana: kuwa na maingiliano ya karibu, kukumbatiana, kupakatana na kupapasana, huondosha vizuizi, hasira na hali ya kukata tamaa. Mara nyingi mtu hupata afueni baada ya kumbatio kubwa, maridhawa.
  10. Zungumzeni mambo mazuri: Iwapo utazungumza na rafiki yako kwa namna unavyozungumza na mwenza wako wa ndoa, je atabaki kuwa rafiki yako? Kuwa mkweli na jibu lako.
  11. Zingatieni usafi kabla ya kulala, na mlale wakati mmoja. Msiendeshe maisha ya kutengana.

HITIMISHO

Ndoa bora ni ile iliyojengwa kwenye msingi wa URAFIKI imara kati ya wanandoa

Mujuni Henry
Author: Mujuni Henry

JUNIITV


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  UMEME WAMWIBUA MWITA WAITARA

Don't miss out!
Invalid email address

Leave a Reply

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading