FIFA YAMKALIA KOONI RAIS WA SOKA HISPANIA

0:00

Zurich

Shirikisho la soka Duniani, FIFA,linapanga kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya Rais wa Shirikisho la soka nchini Uhispania ,Luis Rubiales, kutokana na kitendo alichokionesha wakati wa fainali ya kombe la Dunia la Wanawake siku ya Jumapili.

Rais huyo alimbusu mchezaji wa Timu ya Taifa ya Uhispania, Jenni Hermoso ,mdomoni wakati wa hafla ya kukabidhi tuzo kwa washindi, mara tu baada ya Uhispania kuishinda Uingereza.

FIFA itafanya uchunguzi hili kubaini iwapo vitendo hivyo vinakiuka kifungu cha 13 cha kanuni za nidhamu ,ambacho kinalenga tabia yenye kuudhi na uchezaji wa haki.

Kanuni inasema, hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya yeyote anayekiuka “kanuni za msingi za tabia njema”kumkosea heshima mtu au mwanasheria kwa njia yoyote haswa kwa kutumia ishara au lugha yenye kudhalilisha au “kuonyesha tabia yenye kuharibu sifa ya mchezo wa mpira wa miguu au #FIFA”


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  ALEJANDRO GARNACHO NA TEN HAG WAINGIA KWENYE MGOGORO
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading