BARCELONA YAMUONDOA DANI ALVES KWENYE ORODHA YA NYOTA WAKE

0:00

MICHEZO

Klabu ya Barcelona imemuondoa Dani Alves kwenye orodha ya wachezaji ambao walikuwa wanaheshimika kama magwiji wa klabu katika historia kwenye tovuti rasmi ya klabu ya Barcelona.

Ingawa FC Barcelona haijatoa maoni rasmi, inaaminika kuwa kitendo hicho cha kumuondoa Alves kwenye tovuti kinaashiria kuwepo kwa tahadhari ndani ya klabu kuhusiana na hali anayokumbana nayo Mbrazil huyo kwa sasa baada ya kupatikana na hatia ya unyanyasaji wa kijinsia na kusweka jela kwa kifungo cha miaka 8 na nusu.

Akiwa Barcelona Dan Alves alishinda mataji mbalimbali ambayo yalichochea kazi yake katika umaarufu wa soka. Kando na kuwa mwanasoka hodari, alikonga nyoyo za mashabiki kwa kunyakua mataji Matatu ya Ligi ya Mabingwa, Matatu ya UEFA Super Cups, Matatu ya Kombe la Dunia la Klabu.

Kwa sasa, Dani Alves hatakuwepo tena kwenye tovuti na katika sehemu ya wachezaji wa kihistoria wa Blaugrana, hata hivyo bado haijafahamika iwapo klabu hiyo inaweza kubadilisha uamuzi huo kati yake na mchezaji huyo wa zamani.


Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

See also  FASTEST WAY TO DESTROY YOUR LIFE
Don't miss out!
Invalid email address

By Mujuni Henry

JUNIITV

Please disable your adblocker or whitelist this site!

         banner                            

Discover more from JUNIITV.ONLINE

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading